KWA TAARIFA YAKO: JOSEPH MSAMI -KUTOKA UKONDAKTA MPAKA KAZI UMOJA WA MATAIFA


Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu cha ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu.


Msami na mkewe mpenzi Adela.

"Posta mia hamsini, posta mia hamsini, usivue viatu viatu siti za kulala.. eeh chap chap ndege inaondoka hiyo hakuna kulemba".
Ni sehemu ya maneno ambayo inanijia akilini kumuona Joseph Nichodemus Msami, akiwa kondakta. Sipati picha inakuwaje, lakini ndo hivyo KWA TAARIFA YAKO, Kabla ya haujaanza kutamani kuwa kama yeye ni kwamba pamoja na hapo alipo hivi sasa, Msami ameshafanya kazi ya ukondakta, kuvusha watu kwenye madimbwi kipindi cha mvua maeneo ya sinza, kufundisha driving school, na hata hivi karibuni akiwa BBC, kufanya kazi ya bodaboda.
Pamoja na changamoto ya maisha, Msami hajawahi kukata tamaa, anaeleza jinsi maisha yalivyokuwa magumu wakati nikichat nae alipotinga katika mojawapo ya ofisi za GK, za kaskazini, Arusha (nyingine ikiwa London, na nyingine ikiwa Dar es Salaam)
Ebwana kuna siku mvua inanyesha halafu sasa mteja ni kibonge kuliko mimi, na inabidi nimvushe kwenye dimbwi na hapo sina viatu vya kujiking navyo, si unaijua Sinza ilivyo, full madimbwi kipindi hicho. Kulipa inalipa, sema sasa cha moto utakiona. Anaeleza, Msami,  hapa Napata picha ni nafuu kiroba cha mchanga kuliko uzito mwingine wa walioshiba vema.
Na siku moja kwenye basi kuna mzee mmoja alikuwa ndani, sasa mi nakusanya nauli, anajifanya kuniongelesha kiingereza tu, ha, nilipoona anazidi nami nikaamua kumpa kiigereza change, na nilipoona abiria wengine wananisikiliza, nikapata maconfidence zaidi. Nilimpelekesha yule mzee na kiingereza change cha certificate mpaka akasalimu amri.
Na siku nyingine pia kama kawaida kwenye ruti za daladala, kuna jamaa akapanda alikuwa ni mwandishi wa habari, sasa kwa sababu nilishasoma certificate tayari, na yule mtu namfahamu, aisee ikabidi niishushe kofia chini taaaap, afu ndo nikamgongea nauli, ilikuwa noma sikutaka anione.

Msami akiwa na field work Umaasaini, mkoani Manyara.
KWA TAARIFA YAKO, wanafunzi walikuwa marafiki zangu, sikuwa na ugomvi nao, hicho ni kitu muhimu, na kwa makondakta wengine, usione tabu kufanya hiyo kazi il mradi unajua siku moja utakuja kumiliki gari yako mwenyewe, ama kama una ndoto za kusoma zaidi, wewe kazana huku ukimtumainia Mungu, maana hatakuacha.


Msami kwa hivi sasa, yuko jijini New York nchini Marekani Radio ya Umoja wa Mataifa, yaani UN Radio idhaa ya Kiswahili akiwa ni muandaaji wa vipindi na mtangazaji wa radio hiyo  , lakini kufika kwake hapo ni kutokana na kumuamini Mungu na kutokata tama, ikiwemo kujituma. Ni kama siku moja, kipindi akiwa na shirika la utangazaji wa BBC, kitengo cha Media Action, aliishiwa pesa, na kupiga mahesabu, akaona ni heri pikipiki yake aina ya Bajaj akabebea abiria wawili watatu siku iende. Na hilo lilifanikiwa, kazi ni kazi, hakuna cha umaarufu.


Taarifa ya habari inaletwa kwenu na Josep Msami...

KWA TAARIFA YAKO, mpaka kuja kufikia kuwa mtangazaji mzuri ni kutokana pia na mawazo aliyokuwa nayo tokea utotoni, na hata kugombana na watoto wenzake ili mradi tu asikilize taarifa ya habari. Lakini siku moja, aliipata fresh baada ya kuchapwa sana na mama yake kutokana na kuifungua Redio ili akutane na hao watangazaji anaowasikia kupitia spika. Msami anasema kwamba baada ya hapo, hakurudia tena, ingawa pia mama yake alimnunulia Redio baada kuona kilicho ndani yake.

Hapa ni kukamilisha usajili

Kuufikia U-MC sio shughuli ndogo, lakini aliamini kuwa angeweza kufanikiwa hasa kutokana na kuwa na ushawishi kipindi anapoongea na watu, kuanzia utotoni, mpaka kwenye ukonda, basi akaja kuona kumbe kitu kama hiki kinawezekana. Basi hata uniform za U-MC (viatu) vikatafutwa, na KWA TAARIFA YAKO hivi sasa Msami ni MC ambaye hutojuta kumuita kwenye sherehe yako. Na kuthibitisha hilo, siku ya harusi yake, MC aliyekuwepo alikuwa na kazi ndogo tu, kwani Bwana Harusi alikuwa mchangmshaji kuliko.

Mguu sawa, cadet ndani ya soksi, buti la kazi nje, tayari kwa shughuli ya U-MC
Pamoja na yote ambayo amepitia, ushauri mkuu anaoutoa kwa makondakta wenzake, na kila aina ya mtu amaye anahisi kukata tama ya maisha ni kwamba, ni marufuku kukata tamaa, na huwezi kufikia lengo lako bila kujaribu.
Na kwa kumalizia ni kwamba, KWA TAARIFA YAKO Joseph Msami ni Refa mwenye leseni, ni mwanamichezo, captain wa WAPO SC, Mwandishi wa habari, muendesha bodaboda wa dharura (ambaye muda mwingine inalazimika kusukumwa
* sio tatizo la mafuta) na pia ni MC, na mtafsiri mzuri tu wa mahubiri ya lugha ya kiingereza. Haya yote anasema, kama si kumtumainia Mungu, basi hakuna ambacho kingewezekana.

Captain Msami akimtambulisha mgeni rasmi mwakilishi wa Kamanda wa kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, Marietha Komba, kikosi cha WAPO SC

Producer wa duru za michezo akipokea maagizo kutoka kwa Mhariri Mkuu, wiki moja kabla ya harusi ni ubize kwa kwena mbele



No comments:

Post a Comment